Ramos apewa gari ya thamani kubwa baada ya Real Madrid kuitwanga PSG
- Nahodha wa timu ya Real Madrid, Sergio Ramos alipewa gari kali kama zawadi kwa kuiongoza timu yake kuitandika PSG katika robo fainali ya kombe ya UEFA
- Nduguye Ramos, Rene Ramos alimzawadi nduguye na gari jekundu ambalo kwa upande mwingine ni kama zawadi ya mapema katika kusherehekea siku yake ya kuzaliwa
Nahodha wa timu ya Real Madrid, Sergio Ramos alipokea gari jekundu na la bei ghali kutoka kwa nduguye baada ya kufanikiwa kuing'atua PSG katika kinyang'anyiro cha dimba la kombe kuu barani Uropa.

Habari Nyingine: Wenger afichua atakaposalimu amri kuiongoza Arsenal
Ramos, ambaye anasherehekea siku yake ya kuzaliwa Machi 31 alitumia ukurasa wake wa Istagramu kushukuru kwa gari lake jipya.
"Zawadi za mapema za siku ya kuzaliwa, asante @reneramos." Aliandika katika ujumbe ulioonekana na TUKO.co.ke.
Ramos amefanikiwa kushinda kombe tatu za klabu bora Uropa, nne za La Liga tangu kujiunga na timu hiyo ya Real mwaka wa 2015.
Tuma neno ‘NEWS’ kwa 40227 ili kupata habari muhimu pindi zinapochipuka

Read ENGLISH VERSION
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri: mwangi.muraguri@tuko.co.ke
Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke
Subscribe to watch new videosChanzo: TUKO.co.ke
ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2Bvzmeinmdia4VygpJmqZqln6h6orzEsJhmn5Gntm7FwGaroZmdlruqecqumbCZXZeuorDAZrCaZaKarq15zJqbq6GUYri2tdOwmKefkWK9tLONoaumpA%3D%3D